M23 waelekea mji mwingine wa Butembo, Kongo
19 Februari 2025Mashuhuda na wakazi wa eneo hilo wameelezea mapambano makali katika barabara zinazoelekea katika mji huo huku hali ikizidi kuwa mbaya. Taarifa hiyo imethibitishwa pia na Auguste Kombi, kiongozi wa shirika la kiraia huko Kitsombiro.
Soma pia:UN yawatuhumu waasi Kongo kuwauwa na kuwaandikisha watoto
Hayo yakiarifiwa, msemaji wa jeshi la Uganda Felix Kulayigye amesema kwa makubaliano na serikali ya Kinshasa, wamewatuma wanajeshi wao katika mji mwingine wa mashariki mwa Kongo wa Bunia ili kupambana na wanamgambo wa eneo hilo na kuokoa maisha ya raia.
Bunia ni mji mkuu wa jimbo la Ituri, ambako Uganda tayari ina maelfu ya wanajeshi wanaofanya kazi pamoja na vikosi vya DRC ili kukabiliana na waasi wa ADF wenye mafungamano na kundi la kigaidi linalojiita Dola la Kiislamu IS.