London: Ghasia Sudan huenda zikawa uhalifu dhidi ya binadamu
25 Aprili 2025Lammy, ametoa wito kwa jeshi la serikali na kikosi cha wanamgambo cha RSF kupunguza mapigano haraka, akisisitiza kuwa Uingereza itaendelea kutumia kila njia kuwawajibisha wahusika wa ukatili huo.
Watu 57 wauawa Darfur kufuatia mapigano kati ya jeshi la Sudan na waasi wa RSF
Hali ni mbaya hasa mjini El-Fasher,mji mkuu wa Darfur Kaskazini, ambapo mashambulizi ya RSF yamesababisha vifo vya raia zaidi ya 30 na kujeruhi wengine wengi. El-Fasher ni mji mkubwa wa mwisho wa Darfur unaodhibitiwa na jeshi.
ICC kuomba waranti wa kukamatwa kwa waliohusika na ukatili Darfur Magharibi
Mashirika ya misaada yameonya kuwa huenda mashambulizi ya moja kwa moja dhidi ya mjini huo yakazua vita vya mtaani na kusababisha maelfu kufurushwa, huku UNICEF ikieleza hali hiyo kuwa ni "jahanamu duniani” kwa watototakriban 825,000 waliokwama katika eneo hilo.