Ligi ya Mabingwa: Real Madrid yaipiga Atletico katika debi
5 Machi 2025Matangazo
Atletico ilipoteza fainali zake mbili kwa Real Madrid katika mwaka wa 2014 na 2016 na ikaondolewa mara mbili nyingine walipokutana katika duru ya mtoano -- katika robo fainali ya 2015 na nusu fainali ya 2017. Pia Jumanne, Arsenal ilipiga hatua kubwa kuelekea robo fainali baada ya ushindi wa 7 - 1 ugenini dhidi ya PSV Eindhoven.
Katika usiku mzuri kwa vilabu vya Ligi ya Premier ya England, Aston Villa ilishinda 3 - 1 dhidi ya Club Brugge, na Borussia Dortmund ya Ujerumani ikatoka sare ya 1 - 1 na Lille ya Ufaransa. Hii leo, Paris Saint-Germain itaialika Liverpool, Inter Milan itakuwa ugenini kwa Feyenoord, Benfica itachuwana na Barcelona, na Bayern Munich itawakaribisha Wajerumani wenzao Bayer Leverkusen.