JamiiLibya
Libya yasitisha shughuli za mashirika 10 ya kimataifa
3 Aprili 2025Matangazo
Mashirika yasiyo ya kiserikali ya Baraza la Wakimbizi la Norway, Madaktari Wasio na Mipaka (MSF), Terre des Hommes, CESVI na makundi mengine sita yaliamuriwa kusimamisha shughuli zao nchini Libya huku ofisi zao mjini Tripoli zikifungwa.
Msemaji idara ya usalama wa ndani wa nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika Salem Gheith, amesema mpango unachukuliwa kama kitendo cha hujuma, ambacho kinalenga kubadili muundo wa idadi ya watu na kutishia jamii ya Libya.
Libya imekuwa ikitumiwa na maelfu ya wahamiaji wanaohatarisha maisha yao baharini wakitaka tu kuingia barani Ulaya.