SiasaLebanon
Lebanon yaunda serikali mpya, ya kwanza tangu mwaka 2022
8 Februari 2025Matangazo
Serikali hiyo yenye mawaziri 24 imeheshimu usawa wa kidini kati ya Wakristo na Waislamu, na itakuwa na jukumu kubwa la kushughulikia matatizo ya kiuchumi na kuimarisha usalama kusini mwa Lebabon, baada ya vita kati ya Israel na kundi la Hezbollah.
Utawala mpya wa Lebanon unalenga kupunguza ukaribu na Hezbollah na kuimarisha mahusiano na Saudi Arabia na mataifa mengine ya Ghuba, ambayo yamekuwa na wasiwasi na kufuatia kukua kwa nguvu za kisiasa na kijeshi za Hezbollah katika muongo uliopita.