Korea Kusini lazima ijiondoa katika mitego ya Marekani
22 Agosti 2025Matangazo
Mikutano hiyo inaakisi changamoto za washirika wa Marekani kukabiliana na msimamo wa upande mmoja wa Washington kuhusu biashara, usalama na ushirikiano wa kijeshi.
Mikutano hiyo inafanyika baada ya Korea Kusini na Japan kufikia makubaliano ya kibiashara yaliyowaepusha na ushuru mkubwa uliopangwa na Marekani, kwa masharti ya kuwekeza mabilioni ya dola katika miradi mipya nchini humo.
Trump atangaza mkataba mkubwa wa kibiashara na Japan
Hata hivyo, mtazamo wa Rais Donald Trump unaoongeza masharti katika ushirikiano wa kibiashara na usalama umeibua hofu nchini Korea Kusini kwamba huenda akadai malipo ya juu zaidi kufadhili uwepo wa wanajeshi wa Marekani, licha ya mipango ya kupunguza idadi yao ili kuelekeza nguvu zaidi dhidi ya China.