SiasaKorea Kaskazini
Korea Kaskazini yafanya jaribio la makombora mapya
24 Agosti 2025Matangazo
Shirika la habari la Korea Kaskazini (KCNA) limesema bila kutoa maelezo zaidi kuwa jaribio hilo la Jumamosi limethibitisha kuwa makombora hayo yanao uwezo wa kukabiliana na vitisho vyote vya angani ikiwa ni pamoja na droni na makombora ya masafa.
Mvutano umekuwa ukiongezeka katika siku za hivi karibuni kwenye rasi ya Korea hasa wakati huu Marekani ikifanya luteka ya pamoja ya kijeshi na Korea Kusini huku mkutano ukitarajiwa pia wiki hii kati ya Marais Donald Trump na Lee Jae Myung wa Korea Kusini.