SiasaAsia
K.Kaskazini yafanya jaribio la kombora la masafa marefu
26 Januari 2025Matangazo
Kulingana na Shirika la Habari la taifa KCNA, kombora hilo linaloweza kurushwa kutoka baharini, lilisafiri umbali wa Kilometa 1,500 na kusafiri kwa kipindi cha kati ya sekunde 7,507 na 7,5011 kabla ya kutua katika sehemu iliyolengwa.
Soma zaidi: Korea Kaskazini yarusha makombora ya masafa mafupi kabla ya kurejea kwa Trump
Jaribio hilo ni sehemu ya mipango ya kujenga ulinzi thabiti wa taifa hilo ili kuwa na udhibiti wa kimkakati wenye ufanisi dhidi ya maadui. Taarifa hiyo imesema jaribio hilo la kombora halikuwa na madhara kwa usalama wa mataifa jirani.