Kongo miongoni mwa wanachama wapya wa Baraza la Usalama
4 Juni 2025Mataifa hayo yatachukuwa nafasi za Algeria, Guyana, Sierra Leone, Slovenia na Korea Kusini zinazomaliza muda wao wa kuhudumu mnamo Januari 1, 2026, na kuungana na wanachama wengine watano wasio wa kudumu kwenye baraza hilo ambao ni Denmark, Ugiriki, Pakistan, Panama na Somalia.
Baraza la Usalama latakiwa kuchukua hatua DRCongo
Baraza hilo la Usalama, lenye jukumu la amani na usalama ulimwenguni, lina wanachama 15 ambapo watano kati yao ni wa kudumu.
Mataifa yenye uwanachama wa kudumu ni Uingereza,China, Ufaransa, Urusi na Marekani, ambayo yana kura ya turufu.
Baraza la Usalama lajadili hatima ya mashoga
Wanachama wengine kumi huchaguliwa kwa vipindi vya miaka miwili miwili.
Nchi huchaguliwa kwa kura ya siri, huku viti vikitolewa kutokana na makundi ya kikanda. Mataifa hayo matano yaliyochaguliwa jana Jumanne hayakupingwa.