SiasaMali
Kiongozi wa Kijeshi wa Mali afanya ziara Moscow
24 Juni 2025Matangazo
Jenerali Goita amesema Urusi ni mshirika muhimu katika vita dhidi ya makundi ya itikadi kali ambayo yamekuwa yakiendesha uasi katika taifa hilo la Afrika Magharibi.
Mali na Urusi zilitia pia saini makubaliano ya kushirikiana katika sekta ya nishati ya nyuklia. Chini ya utawala wa kijeshi ulioingia madarakani baada ya mapinduzi ya mwaka 2021, Mali imejitenga na mkoloni wake wa zamani Ufaransa na kuimarisha uhusiano wa karibu na Moscow.