MigogoroKenya
Kikosi kipya cha maafisa wa polisi wa Kenya chafika Haiti
7 Februari 2025Matangazo
Kikosi hicho ambacho wizara ya mambo ya ndani ya Kenya ilisema kinawajumuisha maafisa 144, kililakiwa katika uwanja wa ndege wa Port-au-Prince na waziri mkuu wa mpito Alix Didier Fils-Aime na Leslie Voltaire mkuu wa baraza la mpito la rais.
Hiki hi kikosi cha pili cha kigeni kuwasili Haiti katika siku chache zilizopita kufuatia kuwasili kwa maafisa kutoka Salvadore Jumanne wiki hii.
Kenya inaongoza tume inayolenga kuisaidai polisi ya Haiti kupambana na magenge ya wahalifu yanayodhibiti sehemu kubwa ya nchi ukiwemo mji mkuu Port-au-Prince.