Kijana aliyepigwa risasi kwenye maandamano Kenya yuko hai
18 Juni 2025Matangazo
Jonah Kariuki amesema Jumatano kuwa kijana wake Boniface Kariuki, anapumua kwa msaada wa mashine.
Kariuki amesema amemshuhudia mtoto wake akipumua, na hivyo ana matumaini kuwa atapona.
Amesema Boniface, mwenye umri wa miaka 22, alikuwa anauza barakoa, na sio mhalifu. Wanaharakati na Kariuki siku ya Jumatano waliitaka askari aliyehusika kumfyatulia risasi kijana huyo afunguliwe mashtaka.
Msemaji wa Polisi, Muchiri Nyaga amesema askari aliyempiga risasi Boniface amekamatwa.
Maandamano ya Jumanne yalikuwa yanapinga mauaji holela yanayofanywa na vikosi vya usalama, baada ya mwanablogu Albert Ojwang, kufariki dunia akiwa mikononi mwa polisi.